Vyuo 161 vyafungiwa

Vyuo 161 vyafungiwa

Kufatia ukaguzi ambao ulifanywa kwa agizo la IGP Camilius Wambura kama sehemu ya kudhibiti wimbi la ajali nchini Jeshi la Polisi Tanzania limebaini vyuo 161 vimefanya udanganyifu kwa kutoa mafunzo ya  udereva ambayo haya kidhi vigezo  na kuvifungia vyuo hivyo

Zoezi hilo la uhakiki lilianza January 02,2023 katika vyuo vyote vya udereva Tanzania nakugundulika  vyuo vilivyohakikiwa ni 297 na vyenye sifa ni 134 amesema IGP

“Umefanyika pia ukaguzi wa leseni 20,944 ambazo zimehakikiwa ni sawa na 1.3%, kati ya hizo leseni 17,726 za Madereva zimebainika kuwa na sifa na wamepewa barua ya udhibitisho”alisema IGP Wambura

Pamoja na hayo leseni 3,214 za Madereva zimefutiwa madaraja kutokana madereva wa leseni hizo kuwa  hawana sifa ya kuwa na madaraja C na E kutokana na sababu za kutosomea madaraja stahiki hii ndio sababu ya kupatikana kwa madereva wasio kuwa na viwango na kusababisha ajali.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post