Utajiri Wa Rihanna Wapungua Kwa Kiasi Kikubwa

Utajiri Wa Rihanna Wapungua Kwa Kiasi Kikubwa

Mkali wa Pop kutoka katika visiwa vya Barbados, Rihanna ameripotiwa kuwa utajiri wake umepungua kwa kaisi kikubwa kutokana na baadhi ya miradi yake ya kibiashara kutofanya vizuri kama ilivyotarajiwa.

Ripoti zinaonyesha kuwa utajiri wa nyota huyo umepungua kiasi kikubwa katika kipindi cha mwaka uliopita ambapo umeshuka kutoka dola 1.7 bilioni hadi 1.2 ukipungua kwa dola 500 milioni kutokana na mauzo ya bidhaa zake kushuka.

Mwimbaji huyo amekuwa akielekeza nguvu zaidi kwenye miradi mingine kama vile bidhaa za urembo za Fenty Beauty na chapa ya nguo za ndani ya Savage X Fenty, huku akipunguza shughuli zake za muziki.

Licha ya changamoto za kifedha, msanii huyo ameripotiwa kuwa bado yupo mbali na umasikini kwani bidhaa zake hizo licha ya mauzo kushuka zinazidi kuchangia utajiri wake kurudi kama zamani.

Kwa mujibu wa ripoti ya Express US, Rihanna anamiliki asilimia 50 ya hisa za Fenty Beauty, huku nusu nyingine ikimilikiwa na kampuni kubwa ya kifahari ya Ufaransa, LVMH, inayoongozwa na tajiri Bernard Arnault.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags