Tems aanza mwaka kwa ushindi

Tems aanza mwaka kwa ushindi

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria Tems ameendelea kuonesha makali yake katika kusukuma muziki kwenye mataifa mbalimbali, sasa ametangazwa mshindi kwenye Tuzo za Billboard Woman kwa mwaka 2024.

Licha ya kutangazwa mshindi siku ya jana Jumatano Januari 24, katika tovuti ya Billboard orodha hiyo ya washindi imejumuisha wasanii chipukizi na wanaojituma katika tasnia ya muziki, na wote watakabidhiwa tuzo zao mwezi Machi.



Billboard Woman in Music zinatalajiwa kutokewa Machi 6, mwaka huu katika ukumbi wa ‘YouTube Theater’ ulioko Inglewood, Califonia, ambapo Tems atapokea Tuzo hiyo ya heshima, Ice Spice kupokea Tuzo ya Hit Maker, na Victoria Monét akipokea Tuzo ya Rising Star.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post