Shekh Walid akiri kuwafungisha ndoa Diamond na Zuchu

Shekh Walid akiri kuwafungisha ndoa Diamond na Zuchu

Licha ya kuwa jana Juni 2,2025 Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Kawambwa wakati akizungumza na Mwananchi hakutaka kuongelea suala la ndoa ya Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Zuhura Othman ‘Zuchu’ hatimaye kiongozi huyo wa dini amethibitisha kuwafungisha ndoa mastaa hao wa Bongo Fleva.

Akizungumza na Mwananchi Walid amesema, amewafungisha ndoa miezi mitano iliyopita, ila habari za kuachana yeye hazifahamu.

"Kwanini watu wanapenda watu wengine wazini, Diamondi na Zuchu ni kweli nimewafungisha ndoa mimi toka miezi mitano iliyopita, ila hilo swali lako unaloniuliza kuhusu wameachana mimi silifahamu, sababu kama wangekuwa wameachana Diamondi angekuja kuniambia mimi.

"Vile mlivyoona kwenye mitandao ni kweli ndoa wala sio kiki, ila naona watu wengi wameshtushwa na hii habari,maana mmezoea kuwasema sema Diamondi na Zuchu wazini kila kukicha sasa hili jambo la kheri lishangilieni na kuliombea kheri"amesema Warid

Aidha Walid hakutaka kuzungumzia hatua zilivyoanza hadi akatafutwa kuwafungisha ndoa Diamond na Zuchu na kwanini ilikuwa siri.

"Mimi sitaki kuzungumzia chochote kile ,swali lako nishakujibu kuwa kweli wamefunga ndoa, hayo mambo mengine ya kiundani zaidi sio jukumu langu kuwaelezea," amesema






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags