Shahidi Mwingine Adai Diddy Alimrushia Kisu Cassie

Shahidi Mwingine Adai Diddy Alimrushia Kisu Cassie

Mambo yanazidi kuwa magumu kwa mkali wa Rap kutoka Marekani, Sean "Diddy" Combs, hii ni baada ya mbunifu wa mitindo Bryana Bongolan, ambaye ni rafiki wa karibu (BFF) wa Cassie Ventura kueleza kuwa Diddy alimrushia kisu Cassie.

Jumatano, Juni 4, mbunifu huyo alieleza kuwa Aprili 2016 alikuwa amemtembelea Cassie na kuwa alishtukia Diddy ameingia kwenye nyumba ya Ventura bila ya taarifa na kumtupia kisu Cassie ambaye amewahi kutamba na wimbo wa "Me & U".

Katika tukio lingine, Bongolan alidai kuwa Diddy alimshika na kumining'iniza Cassie kwenye eneo la nje la ghorofa ya 17 akimshutumu kwa maneno makali kabla ya kumtupa kwenye kochi jambo lililosababisha majeraha ya mwili kwa Cassie.

Aidha shahidi huyo aliendelea akisimulia tukio jingine wakati wa upigaji picha huko Malibu mwaka 2016, Diddy alimzungumzia maneno ya kutisha akisema “Mimi ni shetani na naweza kukua,”, jambo lililofanya mbunifu huyo kuwa na wasiwasi na Diddy.

Hata hivyo, wakati wa kusikiliza ushahidi wa Cassie katika siku yake ya tatu alieleza kuwa alikuwa akiweka kisu kwenye kishikio cha mlango kama silaha ya kumkabili Diddy pamoja na kiashiria cha kutambua endapo mtu ameingia nyumbani kwake.



“Nilikuwa napokea ziara nyingi za ghafla kutoka kwa Sean ambapo alikuwa na hasira, na nilitaka kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja kufunga mlango na pia kuwa na silaha," alieleza Ventura mahakama.

Diddy anakabiliwa na mashtaka ya usafirishaji wa binadamu kwa ajili ya ngono, njama ya kihalifu (racketeering), na usafirishaji kwa lengo la kushiriki katika ukahaba. Amekana mashitaka yote na endapo atapatikana na hatia, anaweza kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani.

Utakumbuka Sean "Diddy" Combs alikamatwa Septemba 16, 2024 katika Hoteli ya Park Hyatt, Manhattan, New York na kupelekwa moja kwa moja katika gereza la Metropolitan huko Brooklyn. Kesi yake ilianza kuzikilizwa Mei 5,2025 huku mashahidi zaidi ya 15 wakitoa ushahidi akiwemo Kid Cudi, Mia, Cassie Ventura, mama mzazi wa Cassie na wengineo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags