Njama Zapangwa Kutoa Uhai Wa R. Kelly Gerezani

Njama Zapangwa Kutoa Uhai Wa R. Kelly Gerezani

Timu ya wanasheria wa msanii R. Kelly imewasilisha ombi la dharura kutaka msanii huyo aachiliwe mara moja kutoka gerezani na apewe kifungo cha nyumbani, hii ni baada ya maisha yake kuwa hatarini katika gereza hilo.

Mawakili hao wanadai kuwa kunaushahidi wa wazi unaowalenga maafisa wa polisi kupanga njama ya kumuua Kelly katika gereza la Serikali huko North Carolina, ambapo anatumikia kifungo chake cha miaka 30.

Katika ushahidi wao, waliwasilisha tamko la kiapo kutoka kwa Mikeal Glenn Stine, mfungwa anayetumikia kifungo cha maisha (terminally ill), ambaye alidai kuwa maafisa wa gereza walimshawishi amuue Kelly kwa ahadi ya kuachiwa huru.

Stine aliambiwa kuwa Kelly na mawakili wake walikuwa karibu kufichua taarifa za kuumiza kuhusu ukiukwaji wa haki, zikiwemo madai ya maafisa kuingilia mawasiliano binafsi kati ya mteja na wakili wake.

Aidha aliweka wazi kuwa maafisa walimwambia akikamilisha agizo hilo atashtakiwa kwa mauaji ya Kelly, lakini ushahidi utakaotolewa hautashughulikiwa na hakutakuwa na hatia.

Inaelezwa kuwa, Stine alianza ukaribu na Kelly Machi, 2025, na alikuwa tayari kumuua lakini alibadili maamuzi yake na kumfungukia Kelly kwamba maafisa wa Ofisi ya Magereza walimuagiza kutekeleza mauaji yake.

Wakili wa Kelly anadai kwamba mwezi Juni, walishtuka kuhusu mfungwa mwingine aliyetumwa na maafisa kuwaua Kelly na Stine ambapo wanadai kuwa Kelly yuko hatarini kwa kuwa bado yuko kifungoni gerezani hapo na wafungwa wengine ambao wanaweza kutumika na maafisa hao kutekeleza mauaji yake.

“Tishio kwa maisha ya Bw. Kelly linaendelea kila siku kwamba hakuna hatua zinazochukuliwa,wafungwa zaidi ya wawili waliagizwa kumua Kelly. Zaidi ya mmoja tayari amefikishwa kuhusu kutekeleza mauaji yake. Mmoja wao atafanya kile ambacho Bw. Stine ameshindwa, na hivyo kuzika ukweli kuhusu kile kilichotokea katika kesi hii pamoja na Robert Kelly,” Mawakili waliandika kwenye Jalada hilo.

Wakili wa Kelly, Beau B. Brindley, anamwomba hakimu wa mahakama amuachilie msanii huyo atumikie kifungo cha nyumbani angalau kwa muda mfupi.

Mwimbaji huyo wa R&B, ambaye jina lake halisi ni Robert Sylvester Kelly, alitiwa hatiani kwa makosa tisa ambapo Septemba 2021 alishtakiwa kwa kukiuka Sheria na ulaghai uliohusisha unyanyasaji wa kingono kwa watoto.


Juni, 2022, alihukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani. Pia, Februari 2023, Kelly alihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa ya uhalifu wa kingono kwa watoto, huku hakimu akiamua kwamba muda wote isipokuwa mwaka mmoja atatumikia kwa wakati mmoja na kile kifungo chake cha awali cha miaka 30.

Hata hivyo Februari, 2025, mahakama ya rufaa iliidhinisha hukumu ya Kelly ya ulaghai na ulanguzi wa ngono pamoja na kifungo chake cha miaka 30 jela. Pia, mahakama hiyo ilikataa madai yake kwamba ushahidi wa kesi haukutosha na kwamba hakimu wa kesi hiyo alitoa maamuzi yasiyofaa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags