Naye Saka kukosa mechi mbili za Kitaifa

Naye Saka kukosa mechi mbili za Kitaifa

Mchezaji wa #Arsenal, Bukayo Saka inadaiwa kuwa amejiondoa kwenye kikosi cha ‘timu’ ya taifa ya nchini England kinachojiandaa na ‘mechi’ dhidi ya Australia na Italia.

Nyota huyo wa Arsenal aliyeikosa ‘mechi’ ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Manchester City kwenye ‘ligi’ kuu England, siku ya Jumapili iliyopita kwa sababu ya kuwa majeruhi, lakini inadaiwa amefika kwenye kambi ya Three Lions, St George’s Park.

Baada ya kukutana na madaktari wa timu ya taifa, Saka alijiondoa kwenye kikosi hicho akipewa muda wa kupona majeraha yake yanayomsumbua kwa sasa.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post