Mshindi wa kwanza Mweusi tuzo za Oscar, Sidney Poitier afariki dunia

Mshindi wa kwanza Mweusi tuzo za Oscar, Sidney Poitier afariki dunia

Star wa filamu wa HollyWood, Sidney Poitier amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 94.

Poitier, ambaye alivuka vikwazo vya rangi kama mshindi wa kwanza Mweusi wa mwigizaji bora Oscar kwa jukumu lake katika filamu ya Lilies of the Field, na kuhamasisha kizazi wakati wa harakati za haki za kiraia.

Taarifa za kifo cha msanii huyo kimethibitishwa na Ofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Bahamas, ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa wizara hiyo Eugene Torchon-Newry.

Poitier alitengeneza urithi wa filamu mashuhuri katika mwaka mmoja na filamu tatu za 1967 wakati ambapo ubaguzi ulikuwa umeenea katika sehemu za Marekani.

Katika filamu ya Guess Who's Coming to Dinner aliigiza mtu Mweusi mwenye mchumba mweupe, na "filamu in the heat of the Night alikuwa Virgil Tibbs, Ofisa wa polisi Mweusi aliyekabiliana na ubaguzi wa rangi wakati wa uchunguzi wa mauaji. Pia alicheza kama mwalimu katika shule iliyo na kazi ngumu ya London mwaka huo katika filamu To Sir, With Love.

Poitier alishinda kama mwigizaji bora aliyetengeneza historia ya Oscar katika filamu Lilies of the Field mwaka 1963, akicheza kama fundi ambaye anasaidia watawa wa Kijerumani kujenga kanisa jangwani.

Miaka mitano kabla ya hapo Poitier alikuwa mtu wa kwanza mweusi kuteuliwa katika Oscar kama muigizaji mkuu kwa nafasi yake katika filamu ya The Defiant Ones.

Poitier alipewa heshima ya Knight na Malkia Elizabeth II wa Uingereza mwaka 1974 na aliwahi kuwa balozi wa Bahama nchini Japan na UNESCO, shirika la utamaduni la Umoja wa Mataifa. Pia alihudumu kwenye bodi ya wakurugenzi ya Walt Disney Co kutoka 1994 hadi 2003.

Mwaka 2009, Poitier alitunukiwa tuzo ya juu zaidi ya raia wa Marekani, nishani ya Rais ya Uhuru, na Rais Barack Obama.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post