Mjue Koala, mnyama anayelala saa 22 kwa siku

Mjue Koala, mnyama anayelala saa 22 kwa siku

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya mnyama wa porini aitwaye koala leo Mei 3, jamii imesisitizwa kuhusu umuhimu wa kulala na utunzaji wa mazingira.

Koala ni mnyama wa familia ya wombat ambaye kwa kawaida hupatikana nchini Australia.

Wanajulikana kwa vichwa vyao vikubwa, masikio mafupi yenye manyoya na miili isiyo na mkia na wanachukuliwa kuwa ndiyo alama ya Australia, kama ambavyo twiga huchukuliwa hapa nchini.

Sifa yao kubwa ni kulala sana. Wakati twiga hulala kwa wastani wa saa 1:09 kwa siku, koala hulala kwa kati ya saa 18 hadi 22 kwa siku. Kwa maana nyingine, hupata muda wa kujitafutia chakula kwa saa mbili hadi sita pekee kwa siku.

Siku ya Koala huwaleta pamoja wana mazingira na wanaharakati wa wanyamapori katika kulinda na kuhifadhi mazingira ya koala.

Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post