Mifuko ya hifadhi ya jamii yapewa miezi miwili kulipa madeni

Mifuko ya hifadhi ya jamii yapewa miezi miwili kulipa madeni

Ikiwa ni Siku moja tangu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, kuitaka Serikali kuwawajibisha Waajiri wanaoshindwa kuwasilisha Michango pamoja na Mifuko kutolipa madeni ya Wanachama wake.

Wizara ya Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu imetoa agizo la majina ya waajiri wote sugu wasio wasilisha na wanaodaiwa michango ya wafanyakazi kupelekwa kwa mameneja wa mifuko ya hifadhi ya jamii ndani ya siku 7 kuanzia leo Juni 22, 2023.

Aidha, imeitaka mifuko yote kukamilisha zoezi la kusaini mikataba ya kulipa madeni yote ya michango ya wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii kabla ya juni 30 mwaka huu.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post