Ludacris akumbuka mchango wa Busta

Ludacris akumbuka mchango wa Busta

Rapa kutoka nchini Marekani, Ludacris ametoa shukrani kwa #BustaRhymes kwani ndiyo mtu pekee aliyefanikisha atoke kimuziki.

Kwa mujibu wa Daily Post News Luda ameweka wazi kuwa anaukumbuka na kuuthamini mchango wa Busta kwani asingekuwa na mafanikio yoyote mpaka sasa kama asingekuwepo ‘rapa’ huyo.

Aidha mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 46 hakuweka wazi msaada ambao amewahi kupatiwa na mkongwe huyo lakini ameahidi kumpenda na kumuheshimu siku zote.

Ikumbukwe kuwa wawili hao waliwahi kufanya ngoma za pamoja zikiwemo ‘Throw It Up’, ‘We Must Be Heard’, We Never Miss’, ‘Cannon’ na nyinginezo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post