Nguli wa taarabu Khadija Kopa ambaye ni mama mzazi wa Zuchu licha ya kukanusha kuwepo kwa ndoa kati ya mwanaye na msanii Diamond katika mahojiano mbalimbali, hatimaye Kopa ameiambiwa Mwananchi sababu ya kutohudhuria katika ndoa hiyo.
“Zuhura ameolewa na Diamond japo walifanya siri lakini ni jambo la kheri, kuhusu kutohudhuria kwenye ndoa sisi kama wazazi yaani mimi na baba yake Zuhura tulishatoa ruhusa kama akitaka kufunga ndoa basi afunge tu hata kama sisi hatutakiwepo kiufupi tulitoa baraka zote kwa mtu yeyote atakaye mpata, na vizuri kampata mtu wamefunga ndoa kisirisiri yote kheri
"Nimeona kuna watu wanasema kwanini Shekhe Walid amemshika mkono Diamond na sio Baba yake Zuhura, unajua sisi kama sisi waislamu wakati wowote Shekhe wetu anaweza kuwa Walii kwa upande wa mtoto.
“Na sisi tulishatoa ruhusa kwa Sheikh Walid kuwa ndio Baba yake wa hapa anayemsimamia , hivyo wakati wowote akiwa na jambo la ndoa kwa mtu yeyote Zuhura aende tu kwa Sheikh Walid, na kingine mimi Zuhura nilimzaa nikiwa siko kwenye ndoa ,hivyo kama kuozeshwa angeozeshwa na kaka yake" amesema Khadija Kopa.

Leave a Reply