Utakumbuka kuwa Khan alifunguliwa kesi mwaka 1998 ya uwindaji haramu wa swala mweusi tukio ambalo lilitokea wakati wa utengenezaji wa filamu ya ‘Hum Saath Saath Hain’ katika kijiji cha Kankani, wilayani Jodhpur. Ambapo mwaka 2018 alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela.

Siku ya Jumatano mahakama hiyo ilieleza kuwa mwezi September pia itasikiliza ombo la rufaa ya kuachiwa huru kwa washitaki wenzake na Khan ambao ni Ali Khan, Tabu, Sonali Bendre, Neelam na Dushyant Singh, kesi hiyo inayotarajiwa kusikilizwa na jaji Manoj Kumar Garg.
Aidha wakili wa upande wa mashtaka, Mahipal Bishnoi, alisema kuwa wanasheria wa Salman Khan waliomba kesi hiyo ihamishiwe Mahakama Kuu ili isikilizwe kwa pamoja na ombi la kukata rufaa kwa washtakiwa wengine, lakini mchakato huo hautowezekana kutokana na sababu za kiufundi.
Filamu hiyo ya ‘Hum Saath-Saath Hain’ ambayo imesababisha msala kwa Khan ilitoka rasmi Novemba 5,1999 filamu ambayo iliongozwa na Sooraj R. Barjatya na kuigizwa na mastaa wakubwa wa Bollywood akiwemo Salman Khan, Saif Ali Khan, Tabu, Sonali Bendre, Neelam na wengine.
Leave a Reply