Jinsi ya kukuza biashara yako kutumia mtandao wa kijamii

Jinsi ya kukuza biashara yako kutumia mtandao wa kijamii

Kadri siku zinavyo kwenda mbele basi na mitandao ya kijamii ndivyo huendelea kukua kwa kasi na kukubalika na watu wa kila rika, hivyo basi leo nimekuja na mbinu za kukuza biashara yako kupitia simu yako ya mkononi.

Unaweza kuwa na biashara yako au kampuni yako inayotoa huduma ama bidhaa imara na uhakika kabisa lakini usipotumia bidii kujitangaza ama kujiweka online, unaweza kuzidiwa na watu ambao huduma zao hazina ubora zaidi yako.

Kujitangaza (au kutafuta masoko) kimtandao ni njia rahisi na isiyo na gharama kuwafikia watu wengi zaidi. Ukweli ni kwamba usipofanya matangazo ya biashara yako, yote uyafanyao yataishia kwa watu wachache tu wanaokuzunguka.

Nenda na wakati

Siku hizi mtu akitaka msaada wa jambo Fulani, wazo la kwanza kumjia ni kushika simu yake na kuperuzi kuhusu akitakacho. Hapo ndipo huweza kukutana na majibu ya swala alitakalo mtandaoni.  

Fikiria wewe ndiyo hauko mtandaoni, mtumiaji huyu wa internet atakufahamu vipi? Atafahamu vipi una duka la nguo Kariakoo? Badilika. Nenda na wakati, hamia ulimwengu wa digitali. Wazungu wanaita ‘Digital Marketing’ mbinu ya kutafuta masoko na kujitangaza kupitia majukwaa ya kimtandao kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, email, WhatsApp na kadhalika. 

 

Unaanzia wapi?

Ni rahisi. Ingawa waweza kutumia pesa panapohitajika, kujitangaza mitandaoni ni bure kabisa. Ni kama vile ulivyo na akaunti facebook bila malipo yoyote. Cha msingi ni wewe kujifunza mbinu za uendeshaji na kuchagua njia ipi inakufaa zaidi.

 

Miliki tovuti yako

Tovuti hasa kwa mashirika, makampuni na biashara kubwa ni kitu cha lazima. Hii huongeza hadhi ya kampuni kwa ujumla. Tofauti kubwa kati ya tovuti ama website na mitandao mingine ya kijamii ni namna ya kuweka maudhui. 

Kupitia tovuti, mtu anaweza kupata taarifa kwa kina kuhusu kampuni au bidhaa. 

Pia kwenye tovuti kunaweza kufanyika shughuli kama manunuzi ya mtandaoni, kuandikisha watu kwa ajili ya program, newsletter na kadhalika.

Unatengenezaje tovuti? Ni rahisi. Kuna watu na makampuni mengi yapo kukusaidia kufungua tovuti yako. 

Mitandao ya kijamii

Karibia kila mtu yuko Facebook au Instagram. Maana yake ni kwamba soko liko huko kwa sababu ndiko watu waliko. Cha kufanya ni kupeleka biashara yako huko. Fungua akaunti kwa jina la biashara au kampuni yako na uanze kujitangaza. 

Nini cha kupost ukiwa huko? Hapa ndipo wengi hukosea. Makampuni mengi hapa nchini hayafahamu namna ya kutumia mitandao ya kijamii. 

Mitandao ya kijamii ni watu, hivyo wewe kama kampuni unatakiwa ufahamu namna ya kuishi na watu. Fahamu namna ya kushirikiana na watu. Isiwe kila siku unapost kuhusu wewe na bidhaa zako tu. Utawachosha watu. Kuwa mbunifu. 

Unaweza ukawa unapost picha za bidhaa zako, picha za wateja wenye nyuso za kuridhika na huduma yako. Kama utakuwa mtundu zaidi waweza tengeneza vipande vifupi vya video. Kumbuka pia hautakiwi kupost mara kwa mara ikawa too much.

Jambo la msingi kuzingatia ni kwamba mitandao ya kijamii ni majukwaa tofauti tofauti yenye maudhui na makundi ya watu tofauti. Ni muhimu kulifahamu hili ili aweze kutambua kipi cha kufanya ukiwa kwenye haya majukwaa. 

WhatsApp pia ni fursa kubwa

Kwa kaiwaida WhatsApp hujumuishwa kwenye kundi la mitandao ya kijamii. Lakini kiuchambuzi zaidi, WhatsApp pamoja na majukwaa mengine kama Telegram na Messenger yanaitwa private messaging platforms. WhatsApp imekuwa kimbilio la wajasiriamali wengi wa kitanzania. Kupitia magrupu na status whatsapp, watu wanatangaza bidhaa zao na kupata wanunuzi. 

Weka biashara yako kwenye Google My Business

Kampuni ya Google wana mfumo wa kukuwezesha kuweka biashara yako kwenye ramani ya Google ili watu wa karibu na eneo lako waweze kukuona wakitafuta huduma au bidhaa inayoendana na yako. Pia wanaweza kuacha maoni kama vile kukupa five star rate ili kuongeza visibility yako mtandaoni.

Pia zipo tovuti zingine zinazokuwezesha kuorodhesha biashara au bidhaa yako kama vile Kupatana, na Zoom Tanzania.

Kuwa mbunifu katika maudhui (Content Marketing) 

Karibia kila mtu anaandika maudhui mtandaoni. Iwe ni mstari mmoja kama status za facebook na whatsapp lakini yote ni maudhui. Kinachokuja kutofautisha kati ya maudhui mengi yanayoandikwa kila siku mtandaoni ni aina na stadi za uandaaji maudhui hayo. 

Nichukulie mfano wa mchekeshaji maarufu nchini, Idris Sultan, kuna wakati huandika posts kwenye ukurasa wake wa Instagram akitangaza makampuni kama Uber. Uandishi wake ni mwepesi na wenye ucheshi lakini hapo ameweza kutangaza biashara. 

Kwa makampuni na taasisi mbalimbali unaweza kuajiri muandaa maudhui na mwongozaji wa akaunti za kijamii za kampuni. Hili ni jambo muhimu sana katika ulimwengu wa mawasiliano ya kidigitali.  

Kampuni yetu ina wataalamu wa masuala ya Digital Marketing ambao wanaweza kukurahishia kazi kuandaa yote haya. Kazi yako ni kufanya biashara, sisi tunaimarisha uwepo wako mtandaoni (online visibility) 

Amua sasa!

Siku hizi mambo yanaenda kidigitali, hivyo hata biashara yako haina budi kuenda na wakati. 

Kama uliwahi kujaribu tovuti au mitandao ya kijamii na haukupata matokeo mazuri basi kuna mahali haukufanya kwa usahihi. Tafuta wataalamu wakusaidie.






Comments 3


  • Awesome Image
    DataManics

    To deliver our expertise flexibly and with maximum impact, we have developed different ways of working. Each is adaptable to your core needs, processes, and culture of your business. Find More About Just Click https://datamanics.co.tz/

  • Awesome Image
    Deepak

    Best Digital Marketing Company in Tanzania. Checkout for more information https://datamanics.co.tz/

  • Awesome Image
    Robert Hardie

    Enjoy the best Digital Marketing Services in Tanzania, Just click and explore the right one https://datamanics.co.tz/

Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post