Jezi ya Michael Jordan yavunja rekodi kwa kuuzwa bei ghali

Jezi ya Michael Jordan yavunja rekodi kwa kuuzwa bei ghali

Hellow! I hope mko good watu wangu wa nguvu. Nadhani mnamkumbuka yule mwamba alietamba katika mchezo wa basketball, basi bwana unaambiwa jezi iliyovaliwa 1998 na Micheal Jordan katika fainali ya NBA kati ya timu yake Chicago Bulls na Utah Jazz imevunja rekodi ya jezi ya Maradona kwa kuuzwa bei ghali zaidi ulimwenguni.

Jezi ya Micheal Jordan imeuzwa kwa $10.1millioni, sawa na Bilioni Tsh23.3, ikuvunja rekodi ya mwezi Mei ya jezi aliyoivaa Maradona 1986 wakati Argentina akimfunga England katika mchezo wa robo fainali ya kombe la dunia iliyouzwa kwa $9.3 millioni, sawa na Bilioni Tsh21.7.



Hii imekuwa jezi ya pili katika historia ya NBA kuuzwa kwa gharama ya juu baada ya jezi iliyovaliwa na Kobe 1996-97 kuuzwa kwa $3.7 million, sawa na Bilioni Tsh8.7.

Alooooooh! Haya tuambie ni jezi ya mchezaji gani hapa Tanzania inaweza kuuzwa kwa bei ghali? Dondosha koment yako hapo chini mwanangu sana.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post