Ja Rule awakosoa wanaume wanaovaa jeans za kuchanika

Ja Rule awakosoa wanaume wanaovaa jeans za kuchanika

‘Rapa’ kutoka Marekani, #JaRule amewakosoa wanaume wanaopendelea kuvaa jeans zilizochanika huku akidai kuwa ni mtindo wa zamani.

Kwa mujibu wa tovuti ya Daily Mail News imeeleza kuwa mkongwe huyo wa Hip-hop ameukosoa mtindo huo kwa kuwacheka wanaume ambao bado wanavaa suruali zilizochanika hadi leo.

Ja Rule mwenye umri wa miaka 48 ameonekana hana muda na mtindo wa jeans zilizochanika wala mtindo wowote wa nguo za kuchanika kwa sababu anaona fashion hizo zimepitwa na wakati.

Ikumbukwe kuwa mwanamuziki huyo amewahi kusikia katika vibao vingi ikiwemo ‘Holla, holla’, ‘Clap Back’, ‘Always on Time’, ‘Thug Lovin’, na kuonekana katika filamu kadhaa kama ‘Beef, I’m in love with a Church Girl’.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post