Ice cream inayouzwa tsh 16 milioni

Ice cream inayouzwa tsh 16 milioni

Kampuni inayohusika na utengenezaji wa Ice Cream kutoka nchini Japan ya Cellato imetengeneza ice cream ya bei kubwa zaidi duniani iitwayo ‘Byakuya’, inayogharimu dola 6,696 ambazo ni zaidi ya tsh 16 milioni.

Ice Cream hiyo inakuwa na package yenye vitu vya kifahari ikiwemo truffle (uyoga mweusi) kutoka Alba, Italia, ambayo hugharimu takriban $15,192 kwa kilo.

Aidha kampuni hiyo imepanga kutoa ice cream nyingine zenye gharama zaidi kama vile ‘Champagne’ na ‘Caviar’ katika siku zijazo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post