Juni 6, 2025, katika Mahakama ya Shirikisho ya Manhattan, kesi ya jinai dhidi ya mwanamuziki Sean "Diddy" Combs iliendelea kwa ushahidi wa kushtua kutoka kwa aliyekuwa mpenzi wake, aliyejitambulisha kwa jina la bandia ‘Jane’.
Mwanamke huyo, ambaye anatoa ushahidi ikiwa ni siku yake ya pili mahakamani alisema kuwa yeye na Combs walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kuanzia mwaka 2021 hadi alipokamatwa mwaka 2024.
Akitokwa na machozi wakati yupo kizimbani akitoa ushahidi ameeleza kuwa Diddy alimlazimisha kushiriki kufanya matukio ya kingono yaliyojaa matumizi ya dawa za kulevya na wanaume waliolipwa.
Aidha aliendelea kwa kueleza kuwa rapa huyo alimlazimisha kufanya vitendo hivyo wakati wa hedhi, licha ya kujaribu kujiondoa kwenye matukio hayo kwa kutuma uthibitisho wa pads zenye damu lakini Diddy alikasirika huku akimuita muongo kupitia ujumbe wa sauti uliyosikilizwa mahakamani.
Ambapo alimwambia anywe champagne ili kuendelea na matukio hayo ambayo yanachukua zaidi ya masaa 30 huku tukio la mwisho likifanyika Agosti 2024, kabla ya kukamatwa kwa Combs.
Maelezo yake kuhusu matukio hayo, ambayo alisema Combs aliyaita "usiku wa hoteli," yanafanana sana na yale yanayoitwa "freak offs" yaliyotajwa na mpenzi wa zamani wa Diddy, Casandra "Cassie" Ventura.
Wanawake wote wawili walitoa ushahidi kwamba walilazimishwa kushiriki katika matukio hayo bila hiari yao, madai ambayo mawakili wa Combs wameyakanusha.

Leave a Reply