Hakimi atua Tanzania, Rais wa Yanga ampokea

Hakimi atua Tanzania, Rais wa Yanga ampokea

Rais wa klabu bingwa Tanzania Bara #YangaSC Mhandisi Hersi Said amempokea mgeni wake #AchrafHakimi katika Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro ‘KIA’.

Mchezaji huyu bora kutoka katika klabu ya #PSG ya nchini Ufaransa ameambatana na rafiki zake saba, atakuwa nchini kwa wiki moja huku wakitembelea vivutio mbali mbali vya utalii nchini.

Hata hivyo kumekuwa na utamaduni wa mastaa wakubwa duniani wanaocheza soka la kulipwa baraani Ulaya kutembelea vivutio vya utalii hapa Tanzania akiwemo nyota wa #ManchesterUnited, #SofyanAmrabat ambaye yupo Visiwani Zanzibar kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa msimu.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post