Ethiopia, Mahakama zapewa onyo kutoa vitisho kwa waandishi wa habari za uchunguzi

Ethiopia, Mahakama zapewa onyo kutoa vitisho kwa waandishi wa habari za uchunguzi

Mamlaka ya Vyombo vya Habari vya Ethiopia (EMA) ambayo iko chini ya Serikali imetoa onyo kwa mamlaka nyingine ambazo zimekuwa zikiingilia Uhuru wa Waandishi wa Habari wakiwemo wanaofanya Habari za uchunguzi.
 
Onyo hilo limetokana na malalamiko ya Kituo cha Runinga cha EsatTv  kudai imepokea barua ya Vitisho kutoka Mahakama ya Addisababa  ikiwataka Waandishi wake kuachana na Habari za Uchunguzi

Kwa mujibu wa Taasisi ya “reporters without borders”  (RWB) uhuru wa maoni na vyombo vya Habari chini ya Waziri Mkuu  Abiy Ahmed bado una mgawanyiko ingawa kuna Mabadiliko makubwa kulinganisha na Utawala uliopita. Na  zaidi ya Vyombo vya Habari 200 vilivyopigwa marufuku Vimefunguliwa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post