Baba yake Davido atia neno, mwanaye kukosa Grammy

Baba yake Davido atia neno, mwanaye kukosa Grammy

Baada ya kushindwa kunyakuwa tuzo yoyote katika vipendele vitatu alivyoteuliwa na Grammy mkali wa Afrobeat Davido ameeleza kuwa licha ya kukosa Tuzo hizo baba yake mzazi Adedeji Adeleke anaamini kuwa mwanaye ni mkali.

Kufuatiwa na maohijano yake aliyoyafanya na ‘Rolling Stone’ ameeleza kuwa kuteuliwa pekee kulitosha kabisa kumfanya ajivunie, huku akidai kuwa baada ya kutoka katika Tuzo hizo baba yake alimpigia simu na kumwambia kuwa haijalishi nini kilitokea lakini anaamini mwanaye bado ni ‘Legend’.

Siyo Davido pekee ambaye hakuondoka na Tuzo hizo, wapo mastaa wengine kutoka Nigeria akiwemo Burna Boy, Asake, Ayra na wengineo.

Tuzo za Grammy zilitolewa siku ya Jumapili Februari 4 katika ukumbi wa ‘Crypto.com Arena’ Los Angeles nchini Marekani.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post