Aliyedaiwa kumpiga Mohbad ajisalimisha kituo cha polisi

Aliyedaiwa kumpiga Mohbad ajisalimisha kituo cha polisi

Baada ya ‘polisi’ kutoa tangazo la donge nono kwa atakaye mpata aliyekuwa rafiki wa karibu wa MohBad, Prime Boy hatimaye kijana huyo amejisalimisha mwenyewe kwa jeshi la polisi ikiwa ni saa chache tangu tangazo hilo kutolewa.

Prime Boy kwa sasa yuko kizuizini ambako atakuwa huko kwa ajili ya kuhojiwa na kusaidia uchunguzi kufuatia kifo cha Mohbad, kwani inadaiwa alimpiga kabla ya kifo chake.

Huku polisi jijini humo wakieleza kuwa hakuna ushahidi utakaoachwa kwenye uchunguzi unaoendelea na wote waliohusika na kifo cha msanii huyo watakamatwa na kufikishwa mahakamani.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post