Albumu ya kwanza ya Tems kutoka Juni 7

Albumu ya kwanza ya Tems kutoka Juni 7

Mwanamuziki anayetamba na kibao cha ‘Me & U’ kutoka Nigeria, Tems ametangaza kuachia albumu yake ya kwanza iitwayo ‘Born In The Wild’ inayotarajiwa kutoka Juni 7, 2024.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Tems ameweka wazi tarehe rasmi ya kuachia albumu yake hiyo huku ikiambatana na ziara yake ya dunia aliyoipa jina la ‘Born In The Wild World Tour’ ambayo itaanza Juni 12 jijini London na kutamatika Novemba 15 huko Sydney Australia.


Kwa sasa Tems ameachia ngoma mpya iitwayo ‘Love Me JeJe’ aliyoiachia siku saba zilizopita ikiwa na zaidi ya watazamani milioni 1.2 katika mtandao wa YouTube.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post