Zaidi ya ndoa 50 zafungwa kwa pamoja

Zaidi ya ndoa 50 zafungwa kwa pamoja

Ndoa 51 zimefungwa kwa wakati mmoja katika kanisa katoliki Parokia ya moyo safi bikira Maria, Ungalimited Jijini Arusha ikiwa ni matunda ya hamasa iliyofanywa na kanisa hilo kuwasaidia waishi kulingana na mapenzi ya mungu.

Ujumbe mkubwa uliotolewa wakati wa maadhimisho ni Wanandoa kutakiwa kupinga na kukemea vitendo vya ukatili vinavyotokea katika Jamii.

Aidha Paroko wa Parokia hiyo Padri Festus Magwagwi amewataka kuwa mstari wa mbele kukomesha vitendo vya ukatili kuanzia kwenye ngazi ya familia kwani bila kufanya hivyo italiingiza kanisa kwenye bonde kubwa la mmomonyoko wa maadili.

Chanzo Ayo media






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post