Wezi wavunja na kuiba perfume zanye thamani ya zaidi ya sh 50 milioni

Wezi wavunja na kuiba perfume zanye thamani ya zaidi ya sh 50 milioni

Wezi sita wavunja vioo vya duka la urembo la Macy’s lililopo Northridge, kwa kutumia nyundo na kisha kuiba manukato ya  yenye thamani ya dola 20,000  ambayo ni zaidi ya tsh 50 milioni.

Kupitia video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inaonesha wezi hao wakiwa wameficha nyuso zao kwa kutumia vifaa mbalimbali.

Hata hivyo Afisa Habari wa Polisi wa Los Angeles Tony Im, amedai kuwa wanaendelea kuwasaka wezi hao ambao walitoroka kwa kutumia gari nyeusi aina ya Infinity.

Ikumbukwe kuwa Los Angeles kumekuwa na mfululizo wa matukio ya wizi katika maduka, tangu mwezi Julai mwaka huu.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post