Serikali nchini Australia chini ya Waziri wa Sheria Mark Dreyfus imeanzisha sheria mpya ya kutoa kifungo cha angalau mwaka mmoja (miezi 12) kwa mtu atakayeonesha chuki ya aina yoyote ile.
Kwa mujibu wa Mark anaeleza kuwa kitendo cha chuki kitachukuliwa kama uhalifu huku sababu kubwa ya kufanya uamuzi huo ikitajwa kuwa ni kutokana na ongezeko kubwa la matukio ya chuki dhidi ya Wayahudi.
Hivyo basi ukibainika na hatia ya kuonesha alama ya chuki ya aina yoyote ile utakabiliwa na kifungo hicho huku sheria hiyo ikipinga zaidi vitendo vya ubaguzi wa dini, rangi, kabila wala kwa watu walemavu.
Leave a Reply