Tyson afunguka maendeleo ya afya yake

Tyson afunguka maendeleo ya afya yake

Baada ya kutangaza kupata changamoto ya kiafya kwenye ndege, bondia wa uzani wa juu Mike Tyson, amewaondoa hofu mashabiki wake kwa kueleza kuwa kwa sasa yupo sawa asilimia 100.

#Tyson kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika kuwa anajihisi yupo sawa kwa asilimia 100 lakini ahitaji kumpiga Jake Paul.

#Tyson anatarajia kuingia ulingoni na #JakePaul Julai 20, 2024 katika uwanja wa AT&T, pia pambano hilo litaoneshwa moja kwa moja (live) katika mtandao wa #Netflix.

Ikumbukwe kuwa siku mbili zilizopita #MikeTyson, alipata dharura ya kiafya ndani ya ndege na kupatiwa matibabu humo humo akiwa anatoka Miami kuelekea Los Angeles.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post