Thiago kurudisha majeshi Fluminense FC

Thiago kurudisha majeshi Fluminense FC

Mchezaji wa zamani wa ‘klabu’ ya #PSG, #ThiagoSilva ameamua kurudi kwenye ‘ligi’ kuu ya #Brazil baada ya kuthibitisha kuondoka katika klabu ya #Chelsea mwishoni mwa msimu huu.

Kwa mujibu wa Sky Sport News imeeleza kuwa mchezaji huyo amefanya maamuzi hayo ya kurudi katika ‘timu’ yake ya vijana  ya #Fluminense baada ya kudumu ndani ya miaka 15 kwenye ‘vilabu’ mbalimbali barani Ulaya kama #ACMilan, #PSG na #Chelsea.

Ikumbukwe pia Thiago alitumikia ‘klabu’ yake hiyo ya utotoni kabla ya kwenda Ulaya ambapo kwa sasa #Fluminense imechukua Ubingwa wa bara la Amerika Kusini .

Beki huyo mwenye umri wa miaka 39 liondoka Fluminense mwaka 2007 na kujiunga AC Milan na sasa amerejea ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili hadi mwaka 2026.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post