Mwanamuziki wa Canada, The Weeknd ameandika historia mpya ‘MetLife Stadium’, Marekani kwa kuwa msanii wa kwanza wa kiume mweusi aliyeingiza pesa nyingi zaidi kwenye uwanja huo baada ya kuwavuta mashabiki zaidi ya 163,000 kwa mara tatu mfululizo kupitia ziara yake ya 'After Hours Til Down'
Mafanikio hayo ya kihistoria yanakuja sambamba na Tamasha la Muziki la Mpira wa Magavana lililofanyika wiki iliyopita ambapo Weeknd alifanikiwa kuuza zaidi ya tiketi 40,000 akiwa peke yake.
Maonyesho hayo yalikuwa sehemu ya Ziara ya The Weeknd's After Hours Til Dawn, ambayo tayari imevunja rekodi ya kujaza mashabiki wengi ulimwenguni.
Hata hivyo ziara hizo hushirikiana na Global Citizen ili kuleta mabadiliko ya kijamii kupitia mapato yake. Kwa kila tiketi inayouzwa kwenye ziara hizo, dola 1 hutolewa ili kusaidia watoto wanaoishi mazingira magumu.
Mashabiki pia wanahimizwa kuchukua hatua kupitia jukwaa la Global Citizen kusaidia kumaliza umaskini uliokithiri. Wale wanaoshiriki wana nafasi ya kupata tiketi za bure.

Leave a Reply