Teknolojia inavyoweza kukuza biashara yako

Teknolojia inavyoweza kukuza biashara yako

Oooooooooooh! Valentine imeshapita sasa haya turudi katika biashara jamani, kama nawaona wauza maua na cake walivyozikusanya pesa week hii, sio powa yaaani mwendo ndo ule ule ni kujishughulisha tuu mpaka pesa zenyewe zichanganyikiwe.

Basi bwana katika ulimwengu huu wa teknolojia, mambo mengi sana yameweza kurahisishwa na hata kupelekea uongezekaji wa ufanisi katika utendaji kazi na hata kuchangia katika kuboreshwa kwa mawasiliano na mengine mengi.

Biashara ni miongoni mwa maeneo ambayo yamepata kukua kwa kasi Zaidi, katika zama hizi za teknolojia biashara nyingi zimekuwa zikifanyika mtandaoni na kurahisisha ulipaji na uwasilishaji wa bidhaa au huduma kwa wakati. Hii yote ni kutokana na ukuaji wa teknolojia.

Na biashara siku hizi haiwezi kwenda bila ya kuwa na teknolojia kwasababu ndo kila kitu kwenye mihangaiko yako ya kutafta rizki, waswahili wenyewe wanasema kosa vyote usikose simu wala bando.

Na haya ndo baadhi ya matumizi ya teknolojia katika biashara yako

  • Kwanza Matangazo

Teknolojia inakuwezesha kutengeneza matangazo ya aina mbalimbali kwa ajili ya kuitangaza biashara yako mfano video na vipeperushi .Pia kwa kutumia teknolojia ni rahisi sana kuitangaza biashara yako katika mitandao ya kijamii, kwenye televisheni au hata radio na magazeti.

  • Pili Mauzo na manunuzi

Unaweza kutumia teknolojia katika kuratibu au kusimamia mauzo na manunuzi yote katika biashara yako. Hii ni kwa kutumia mifumo maalum iliyoundwa kwa kazi hiyo.

  • Tatu Kukusanya wateja

Kupitia barua pepe (email)  ni rahisi zaidi kuwaweka wateja wako karibu zaidi na biashara yako. Pia unaweza kutumia mitandao ya kijamii, kukusanya wateja wako sehemu moja na kuwaweka karibu zaidi kwa kutengeneza makundi au kurasa zinazohusiana na huduma au bidhaa zako. Kufanya hivi kutakusaidia kuwa na wateja au wafuatiliaji wa kudumu wa bidhaa na huduma zako.

  • Nne Ushirikiano na wafanyabiashara wenzako na wafanyakazi wako.

Kutumia teknolojia bwana inakupa urahisi kushirikiana na wafanyabiashara wengine au wawekezaji, katika kuhakikisha masuala ya kibiashara na mipango mbalimbali inakwenda sawa. Mfano, kufanya vikao mbalimbali vya kibiashara kwa njia ya video au sauti, siku hizi watu wengi hutumia (ZOOM) hii itasaidia  kutoa mafunzo mbalimbali kwa njia ya mtandao kwa wateja au wafanyakazi wako.

Pia itakurahisishia katika kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na biashara yako katika mitandao na kujiongezea maarifa zaidi.

  • Tano Kuongeza ufanisi

Itakusaidia kuongeza ufanisi wa biashara yako, mfano utunzaji wa kumbukumbu za mauzo na manunuzi, katika kuwasiliana na wateja wako, Kufanya mauzo na manunuzi, kupokea order(oda) mbalimbali na kufanya delivery(uwasilishaji).

  • Sita Huduma kwa wateja.

Unaweza kutumia teknolojia kurahisisha suala la huduma kwa wateja. Mfano unaweza tumia teknolojia kuboresha mawasiliano na wateja, kuboresha namna ya kuchangamana na wateja(Mfano. kwa kutumia aplikesheni (online customer care agents)) katika kujibu maswali ya changamoto mbalimbali wateja wanazokumbana nazo, au katika kuwapatia maelekezo mbalimbali.

Urahisi katika utafutaji na uagizaji wa bidhaa mpya. unaweza kununua kitu hata nje ya nchi kwa kukiona kwenye mitandao ya kijamii, au tovuti za kibiashara mfano. Ebay, Amazon, AliExpress n.k na ukafanya malipo yote mtandaoni na ukatumiwa hadi ulipo ndani ya muda mfupi.

Haya haya siku hizi tunasema roho ya mungu ila vilivyobaki vyote vya mzungu sio powa kabisa, ni matumaini yangu sijawaangusha watu wangu wa nguvu, sisi hapa tupo kwaajili ya kukujuza mengi kuhusu biashara, elimu, burudani, afya na mengineyo, usiache kufuatilia mitandao yetu ya kijamii @Mwananchiscoop kujifunza Zaidi.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post