Seaun adai Nigeria wamewekeza zaidi kwenye muziki sio elimu

Seaun adai Nigeria wamewekeza zaidi kwenye muziki sio elimu

Mwanamuziki mkongwe nchini #Nigeria, #SeunKuti amedai kuwa muziki wa Nigeria unafanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sababu wamewekeza pesa nyingi kwenye muziki na sio elimu.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo #SeunKuti ameeleza kuwa mafanikio ya muziki Nigeria ni kutokana na kuwekeza pesa nyingi huku akidai kuwa wasanii wengi nchini humo hulipa watu kwa dola kuwafanyia promotion na kuweka muziki wao kwenye nafasi nzuri duniani.

Hata hivyo amekiri kuwa wao sio kwamba wana wasanii bora zaidi duniani ila tu wamefanikiwa kuwekeza kwenye burudani kuliko elimu,

Ikumbukwe kuwa mwaka 2018, msanii huyo alishinda katika Tuzo za Grammys, katika kipengele cha muziki bora ulimwenguni.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post