Sajent Ataka Kurudi Shule Dsquare Fundi Aeleza

Sajent Ataka Kurudi Shule Dsquare Fundi Aeleza

Ibrahim ‘Dsquare Fundi’ ambaye ni meneja na DJ wa msanii wa Singeli nchini Mdogo Sajent ameeleza anayoyapitia msanii huyo kufuatia maneno ya watu kuwa hajui kuimba.

Akizungumza na Mwananchi, Dsquare Fundi amekiri kuwa wakati wa mikwaruzano ya Sajent na Paten msanii huyo alikuwa akiathirika pakubwa hasa alipokuwa akiambiwa hajui kuimba.

“Kila msanii hicho kitu huwa kinamtokea sio kwa yeye tu kwa sababu hata juzi kati tumeona Bro Alikiba anasemwa vibaya hivyo kwa upande wake ni changamoto za maisha kwa hiyo na imani mashabiki wanatakiwa waelewe kuwa wakisema hajui kuimba wanamdidimiza kisanii.

Komenti kama hizo kwenye mitandao ya kijamii zinamuathiri lakini sasa itabidi azoee apambane, komenti zipo na zitaendelea kuwepo, maneno yalivyomuandama kipindi kile nilikuwa simpagii simu kwa sababu hakuwa sawa nilikuwa namshauri apotezee na apambane afanye muziki,”amesema Dsquare Fundi

Aeleza alipokutana na Sajent

“Sajent ni ndugu yangu nakumbuka aliletwa nyumbani tukae naye, akaniambia kuwa anapenda kuimba nikamsikiliza kwa hiyo nilivyomsikiliza kipindi hicho alikuwa anaimba bakora, nikamwambia kuwa unajua lakini muziki huu sio muziki na hautakupa pesa hivyo nikamshauri ageukie kwenye singeli ilia pate pesa.

Sina undugu wowote na yeye naweza kusema ni mdogo wangu nilikuwa ninakaa naye nyumbani pale tunapoishi watu wengi ni wamuziki hivyo aliletwa kipindi bado sijamaliza shule mwaka 2019,”amesema Meneja Sajent.

Aidha akizungumzia kuhusu kusoma ameeleza kuwa “Hasomi baada ya kumpoteza mama yake mambo yakawa hayaendi vizuri akashindwa kuendelea na shule. Yeye mwenyewe Sajenti anahitaji kurudi shule kwahiyo ndio tupo kwenye process."

Mbali na watu kumnanga kupitia ngoma zake kwa sasa Mdogo Sajent anafanya kazi akishirikiana na Chino Kidd huku wakitoa wimbo wa pamoja uitwao ‘Tunakuja kama Mazombi’ .






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags