Rema atimiza ndoto yake ampata Ice Spice

Rema atimiza ndoto yake ampata Ice Spice

Baada ya mwanamuziki kutoka nchini Nigeria, Rema kueleza ndoto yake ya kuendelea kufanya ‘kolabo’ na ma-star mbalimbali kutoka Marekani, hatimaye ndoto yake ya kwanza imetimia baada ya msaniii wa hip-hop Ice Spice kutoka nchini humo kutangaza kuachia ngoma na Rema.

Kupitia ukurasa wa X wa Ice Spice ame-share picha ya cover ya wimbo huo, akiwa ameandika Pretty girl ft Rema ambao utatoka Ijumaa ya week hii.

Ikumbukwe mshindi huyo wa tuzo ya MTV kufuatia mahojiano yake alieleza kuwa ndoto yake ni kuendelea kufanya ‘kolabo’ na wanamuziki wakubwa kutoka Marekani akiwemo, Megan Thee Stallion, Ice Spice na wengineo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post