Nini kinaendelea nyuma ya tweets za Barbara

Nini kinaendelea nyuma ya tweets za Barbara

Mfanyabiashara na aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa ‘Klabu’ ya Soka Tanzania, Simba Sport Club, Barbara Gonzalez, ameendelea kuacha maswali kwa mashabiki wa soka nchini kutokana na #Tweets zake anazoendelea ku-share kwa followers wake kwenye mtandao #Twitter.

Tangu siku mbili zilizopita #Barbara amekuwa ni mtu wa kutwees mafumbo ambayo watu wanajiuliza na kushindwa kuyafumbua kile anacho maanisha.

Kwenye Tweet ya kwanza Barbara aliandika, “Hauwezi kudhulumu haki za watu halafu ukataka amani na mafanikio” na iliyofata akaandika, “Usilipize ubaya kwa ubaya lakini usiwe mnyonge kudai haki zako”.

Lakini pia leo hii mfanyabiashara huyo ame-tweet ujumbe usemao,  “Ulevi wa madaraka haujawahi kuwa na mwisho mwema”.

Je unahisi nini kinaendelea nyuma ya #Tweets za Barbara, madongo ya hayo ni kwa Simba au #MohammedDewji






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post