Mwigizaji Johnny Wactor afariki dunia

Mwigizaji Johnny Wactor afariki dunia

Mwigizaji kutoka Marekani Johnny Wactor ambaye alijulikana zaidi kupitia tamthilia ya ‘General Hospital’ amefariki dunia kwa kupigwa risasi katika moja ya mtaa wa Los Angeles.

Taarifa ya kifo chake imetolewa na mama yake mzazi Scarlett Wactor ambapo aliviambia vyombo vya habari siku ya jana Jumapili Mei, 26, 2024 kuwa mwanaye alipigwa risasi na wezi watatu waliotaka kuiba kwenye gari lake siku ya Jumamosi asubuhi.

Wactor amefariki akiwa na umri wa miaka 37, huku akionekana kwenye tamthilia kama ‘Lifetime’, ‘Lifetime’, ‘Hollywood Girl’, ‘Hollywood Girl’, ‘The Passenger’ na nyinginezo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post