Mwalimu akamatwa kwa kesi ya ubakaji wanafunzi

Mwalimu akamatwa kwa kesi ya ubakaji wanafunzi

Mwalimu wa madrasa (chuo cha kislam) nchini Senegal anayeshukiwa kuwabaka wanafunzi wake 27 wa kike, amekamwatwa  siku ya jana Jumatatu baada ya kulikimbia jeshi la polisi.

Mwalimu (Ostadhi) huyo anatuhumiwa kuwabaka wanafunzi katika madrasa yake katika mji mtakatifu wa Touba afisa wa polisi wa mji huo amesema.

Mshukiwa huyo alitoweka baada ya tuhuma hizo kuibuka mapema mwaka huu kufuatia malalamiko kutoka kwa watu wanaodaiwa kuwa waathirika waliotoa vyeti vya matibabu

 Aidha mtuhumiwa alitiwa nguvuni na jeshi la polisi siku ya Jumatatu baada ya kujisalimisha kwa polisi.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post