Mbakaji aachiliwa huru baada ya kukubali kumuoa muathiriwa

Mbakaji aachiliwa huru baada ya kukubali kumuoa muathiriwa

Mahakama ya Pakistan imemwachilia mbakaji baada ya kukubaliana kumuoa mwathiriwa wake katika suluhu iliyosimamiwa na baraza la wazee kaskazini-magharibi mwa nchi hiyo, kulingana na wakili wake.

Uamuzi huo umewakasirisha wanaharakati wa haki, ambao wanasema unahalalisha unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake katika nchi ambayo ubakaji mwingi hauripotiwi.

Dawlat Khan, 25, alihukumiwa mwezi Mei kifungo cha maisha jela na mahakama ya chini katika wilaya ya Buner katika jimbo la Khyber Pakhtunkhwa kwa kumbaka mwanamke mwenye ulemavu wa kusikia.

Aliachiliwa kutoka gerezani Jumatatu baada ya Mahakama Kuu ya Peshawar kukubali suluhu nje ya mahakama iliyokubaliwa na familia ya manusura wa ubakaji.

"Mbakaji na mwathiriwa wanatoka katika familia moja," Amjad Ali, wakili wa Khan, aliiambia AFP.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post