Mandonga apokea kichapo Kenya

Mandonga apokea kichapo Kenya

Bondia Karim Mandonga  akili kupokea kipigo kutoka kwa Bingwa wa Zamani wa Mkanda wa #Africa Boxing Union (ABU), Daniel Wanyonyi kutoka nchini Kenya.

Wanyonyi amemdunda #KarimMandonga mtu kazi kwenye pambano la marudiano lisilo la ubingwa lililofanyika Jumamosi kwenye ukumbi wa Sarit Centre Expo jijini Nairobi.

Mandonga amedai kuwa Wanyonyi alikuwa bora ndiyo maana ameshinda mpambano huo, lakini kama ilivyo kawaida ya Mtu Kazi,   hakuacha kujitapa kwa kusema kuwa yupo tayari kwa mpambano watatu ambao watarudiana na mpinzani wake.

Kwa upande wa Wanyoni imekuwa furaha kwa ushindi aliyoupata huku akidai kuwa ushindi wake umetokana na kufanya mazoezi.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post