Madhara ya kuvaa Miwani ya urembo

Madhara ya kuvaa Miwani ya urembo

Na Aisha Lungato

Mambo vipi mtu wangu wa nguvu, leo bwana katika urembo na fashion tunakuletea athari za kuvaa miwani za urembo maarufu kama miwani za jua, kwa siku za hivi karibuni imeonekana vijana wengi hupendelea kuvaa miwani hiyo bila kujua madhara yake, miwani hiyo imetajwa kuwa na madhara kwa watumiaji wake kutokana na watu kutofahamu size za namba ambazo wanapaswa kuzivaa kabla ya kununua.

Akifafanua kwenye kipindi cha Supamix kinachorushwa East Africa Redio, Daktari bingwa wa upasuaji wa macho kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk. Neema Daniel Kanyaro amesema watu wengi amekuwa wakivaa miwani pasipokujua kwamba zinaweza kuwasababishia matatizo ya kuona.

Dk. Kanyaro amesema kwamba watu wamekuwa wakivaa miwani za jua kama urembo pasipo kwenda kupima kujua ni aina gani ya miwani wanazotakiwa kuzitumia lakini pia bila kujua kama miwani hizo zina namba ambazo kila mtu ana namba kutokana na uono wake.

"Miwani ni dawa lakini usivae bila kupima kwani inaweza kukusababishia matatizo ikiwemo uoni hafifu. Unaweza kukuta unavaa miweani nyeusi lakini kumbe siyo namba yako. Kama hujijui unaweza kuta ukitazama unaona giza kumbe umeshaua macho kwa urembo," amesema.

Akizungumzia kuhsu presha ya macho, Dk. Kanyaro amesema kwamba ugonjwa huo hauna dalili za moja kwa moja bali ni lazima kupima na huathiri watu wa rika zote.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post