Lulu amjia juu shabiki kisa Hamisa Mobetto

Lulu amjia juu shabiki kisa Hamisa Mobetto

Muingizaji wa #BongoMovie Elizabeth Michael (Lulu), kama ilivyo kawaida yake kutovumilia maneno ya  mashabiki kwenye mitandao ya kijamii, kwa mara nyingine tena #Lulu amamjia juu shabiki aliye-comment kwenye ukurasa wake wa #Instagram na kudai kuwa #Lulu anamuonea wivu #HamisaMobetto.

Siku ya jana #Lulu ali-post picha ya mwanae wa kwanza na  kumtakia heri ya siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa, ndipo shabiki huyo alishusha comment kwenye picha hiyo na kuandika, “Range za Hamisa zinakutoa roho, imebidi upost mtoto”,

 kama ilivyo kawaida ya #Lulu kutovumilia maneno ya mashabiki alimjia juu shabiki huyo na kuandika,  “Wapenda kujipa umuhimu hao wanahisi kila mtu ni fan wa mabati, wengine sehemu za kutu google ni ardhi huko, wanaweza kufa tumenunua mpaka wanapolala”.

Maneno hayo yamekuja mara baada ya #Hamisa kupost gari lake jipya aina ya #Range ambalo anamiliki sasa, hata hivyo nikukumbushe kuwa #Hamisa ni mazazi mwenzie na #Majizzo ambaye ni mume wa #Lulu






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post