Ligi yasimamishwa baada ya muamuzi kushambuliwa

Ligi yasimamishwa baada ya muamuzi kushambuliwa

‘Ligi’ ya nchini Uturuki yasimamishwa baada ya muamuzi, Halil Umut kushambuliwa ndani ya uwanja katika ‘mechi’ iliyochezwa usiku wa Jumatatu dhidi ya #Rizespor na #Ankaragucu.

Tukio hilo lilitokea baada ya Rais wa ‘klabu’ ya #Ankaragucu, #FarukKoca kumpiga ngumi refa huyo uwanjani na kusababisha fujo baada ya mchezaji wa Rizespor, #AdolfoGaich, kufunga bao la kusawazisha dakika ya 97.

Kufuatia tukio hilo, Rais wa Shirikisho la Soka la Uturuki ametangaza kusimama kwa shughuli zote za mpira wa miguu nchini humo kwa muda usiojulikana.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post