Jana Machi 23, 2025 picha ya mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii huku ikiwashangaza wengi kutokana na bei inayouzwa.
Picha hiyo ilipigwa na Getty Images Juni 21, 2025, katika tamasha kubwa la muziki nchini Marekani, Hot 97 Summer Jam na kupigwa mnada kwa dola 499 'sh1.3 milioni' ikiwa na ubora wa juu (4188 x 6000px| 25.1MP).
Huku ya ubora wa chini kabisa dola 150 'sh391,000' na ubora wa kati ni dola 350 sh 912,000/=
Hii sio mara ya kwanza kwa Getty Image kumpiga picha msanii huyo, mwaka 2015 walimpiga picha kwenye usiku wa tuzo za BET Awards. Tena walimpiga wakati wa tuzo za MTV Afrika Music Awards (MAMA 2015). Ambapo katika tuzo hizo Diamond alifanikiwa kushinda kipengele cha Best African/Indian Act.
Diamond siyo msanii pekee wa Bongo Fleva aliyewahi kupigwa picha na Getty Image, kwani mwaka 2015 ilitokea kwa Vannessa Mdee katika tuzo za BET. Pia Abigail Chams alipigwa picha kwenye BET Awards 2025.
Tofauti na wanamuziki mchezaji wa soka Mbwana Ali Sammata alipigwa picha na Getty Image kwenye matukio ya mechi mbalimbali, kama ile wakati akifunga goli la kichwa kwenye mechi ya champitions League Liverpool vs Genk 2019.
Kwa upande wa wasanii wa Afrika kiujumla wapo wengi wambao wamewahi kupigwa picha na Getty Image tangu miaka ya 2010 yupo Wizkid, Burna Boy, Davido, na Black Coffee, ambapo picha hizo zilipigwa wakati wakiwa kwenye matukio kama tuzo, pafomansi, na shughuli nyingine kubwa za muziki.
Kumbuka, Getty Images ni kampuni kubwa ya kimataifa inayojihusisha kupiga, kusambaza na kuuza picha zenye ubora wa hali ya juu kwa vyombo vya habari, wafanyabiashara na watu binafsi.
Wanapiga picha watu maarufu, viongozi, wanamichezo na wasanii kwa sababu watu hao wanaushawishi mkubwa na picha zao zinathamani kubwa sokoni. Pia wanachagua matukio makubwa kama Tuzo, Matamasha na Hafla rasmi ili kupata picha zenye mvuto wa kibiashara kwenye soko la duniani.
Kwa ujumla, hatua hii inaonesha wazi jinsi thamani na hadhi kubwa aliyofikia Diamond Platnumz kwenye ramani ya Muziki Duniani.

Leave a Reply