Kodak kuondoa laana ya kwenda jela kila mwaka

Kodak kuondoa laana ya kwenda jela kila mwaka

Rapa kutokea nchini Marekani Kodak Black amefunguka na kusema kuwa hajawahi kumaliza mwaka bila kwenda jela tangu awe na umri wa miaka 14.

Unaambiwa kuwa kwa sasa anataka kuiondoa laana na mkosi huo wa kwenda gerezani kila mwaka.

Kupitia Insta Story yake mwanamuziki huyo amefunguka na kusema kuwa kwa sasa ameshamalizana na maisha ya aina hiyo ya kumpeleka jela na sasa ataelekeza maisha yake kwenye muziki zaidi.

Hebu tuambie msomaji wetu unadhani mwaka huu mpya wa 2022 ni mwaka wake kweli na malengo yake hayo yanaweza kutimia.

Tuandikie maoni yako hapo chini na kwenye ukurasa wetu wa Instagram ambao ni @MwananchiScoop.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post