Internet yazimwa kwa muda Pakistan

Internet yazimwa kwa muda Pakistan

Huduma za Internet nchini Pakistan zimezuiwa kwa muda kuhofia ugaidi wakati wa zoezi la uchaguzi linaloendelea leo nchini humo kufuatiwa na upinzani mkubwa wa vyama viwili vya siasa ambavyo ni OML-N na PPP.

Kwa mujibu wa #ArabNews inaeleza kuwa wizara ya mambo ya ndani nchini humo imesema kuwa hatua hiyo imetolewa kutokana na kuwepo kwa viashiria vya ugaidi wakati wa uchaguzi.

Aidha kufuatiwa na uamuzi huo mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani Bilawal Bhutto, Zadari Bhutto ameikosoa hatua hiyo kwa kusema kuwa serikali inapaswa kuachia huduma hizo kwa jamii haraka iwezekanavyo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post