FAIDA ZA KARANGA MBICHI KIAFYA

FAIDA ZA KARANGA MBICHI KIAFYA

Karanga ni moja ya vyakula katika kundi la Legumes (Kunde). Tokea zamani babu zetu walitumia karanga kama chakula na hasa wanaume walizitumia zaidi kwasababu walitambua umuhimu wa karanga katika afya yao.

Kutokana na umuhimu mkubwa na faida za karanga kwa afya za wanaume, Inashauriwa Kwa mwanaume aliyeoa kula karanga angalau nusu ya kiganja cha mkono wake kila siku, ila kwa ambao hawajaoa inashauriwa wale angalau robo kilo kwa wiki moja.

Karanga zenyewe ni nzuri kama vitafunio. Koroa-kukaanga na chumvi au pilipili, karibu kila wakati huonekana kwenye meza za baa na mbele ya baa.

Kila kitu kiko wazi hapa: chumvi huchochea hamu ya kunywa zaidi, na kwa vitafunio vile vya bure, unaagiza vinywaji vingi kuliko vile ulivyotarajia.

Nchini India, karanga hukaangwa kaskazini na huchemshwa kusini. Imepikwa na mchanganyiko wa manukato ya Sichuan nchini China, na huko Merika, karanga za kuchemsha ni vitafunio maarufu katika majimbo ya kusini.

Hapa, karanga ni maarufu kutengeneza bamba ya karanga na siagi ya karanga, bila ambayo hakuna kifungua kinywa.

Nchini Indonesia, saladi za jadi huchafuliwa na mchuzi wa karanga; kusema juu ya Mali na Zambia, mboga mboga na kuku wa kukaanga hutiwa siagi ya karanga iliyochanganywa na vitunguu na vitunguu; wakati huko Mauritius, ni kawaida kupaka karanga za kuchoma kama ishara ya ustawi; nchini Mali, imeongezwa kwa sungura iliyokaliwa.

Kwanza kabisa karanga husaidia katika kutibu magonjwa ya moyo

Kama ilivyokuwa kwa korosho, karanga nazo ni chanzo kizuri cha mafuta mazuri aina ya monounsaturated fats’ ambayo yanatiliwa mkazo kutumiwa kwa afya ya moyo.

Kwa mujibu wa utafiti, watu wanaokula karanga mara kwa mara hupunguza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo (cardiovascular heart disease).

Aidha, katika taarifa iliyochapishwa kwenye jarida moja la Uingereza la ‘Journal of Nutrition’ ambako kuna matokeo ya taarifa nne za utafiti, imeonesha pia watu wanaotumia karanga mara kwa mara, angalau mara nne kwa wiki, hujipa kinga nyingine dhidi ya ugonjwa wa moyo (coronary heart disease) kwa zaidi ya asilimia 37.

Mbali ya kuwa na mafuta mazuri yanayotoa kinga kwenye moyo, karanga pia, zinaelezwa kuwa na kiwango kikubwa cha virutubisho vinavyotoa kinga ya mwili (antioxidants) kuliko hata kile kinachopatikana kwenye tunda la epo na karoti!

Ili kupata kinga hiyo dhidi ya aina hizo mbili za ugonjwa wa moyo, ambao unatesa watu wengi duniani na kugharimu pesa nyingi kwa matibabu, unashauriwa kula karanga pamoja na bidhaa zake kama vile peanut butter, angalau kijiko kimoja cha chakula, mara nne kwa wiki.

 

  1. Kinga dhidi ya kiharusi.

Ugonjwa mwingine hatari unaosumbua watu wengi hivi sasa ni kiharusi au stroke’, lakini unaweza kujikinga nao kwa kuwa na mazoea ya kula karanga tu.

Utafiti umeonesha kuwa karanga ina kirutubisho aina ya Resveratrol ambacho hupatikana pia kwenye zabibu na mvinyo mwekundu (red wine). Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa maabara na kuchapishwa kwenye jarida la Kilimo na Kemia ya Chakula (Journal of Agricultural Food Chemistry),umeonesha kuwa kirutubisho hicho huimarisha utembeaji wa damu kwenye mishipa inayokwenda kwenye ubongo kwa kiasi cha asilimia 30.

3. Kinga dhidi ya magonjwa ya moyo.

Faida nyingine inayoweza kupatikana kwenye mwili kutokana na ulaji wa karanga, ni kinga dhidi ya ugonjwa wa saratani ya tumbo. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa, unaonesha kuwa virutubisho vya folic acid, phytosterols, phytic acid’ (inositol hexaphosphate) na resveratrol’ vinavyopatikana kwenye karanga, huweza kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa saratani ya tumbo.

Zaidi utafiti huo umeonesha kuwa ulaji wa karanga hata mara mbili tu kwa wiki, una uwezo wa kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani ya tumbo kwa asilimia 58 kwa wanawake na asilimia 27 kwa wanaume. Kwa maelezo hayo kuhusu faida za karanga mwilini  bila shaka chakula hiki kinapaswa kupewa kipaumbele katika orodha ya vyakula tunavyokula.

kila siku na hakika Mungu ametupenda sana kwakutupa kinga dhidi ya maradhi yote yanayotukabili kwa njia ya vyakula






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post