Fahamu baadhi ya Mataifa  yenye idadi kubwa ya watu.

Fahamu baadhi ya Mataifa yenye idadi kubwa ya watu.

Haishangazi sana kuona  nchi kubwa zaidi ulimwenguni zinaongoza kiuchumi pia kuwa  na idadi ya watu wengi, mataifa kama china na India yanaongoza kwa  idadi  ya kuwa na watu wengi  zaidi ya bilioni .

Marekani inashika nafasi ya tatu ikiwa na wakazi zaidi ya milioni 335. Nchi za BRIC (Brazil, Russia, India na China), kwa ujumla zinazochukuliwa kuwa nchi nne kuu zinazoinukia kiuchumi ambazo zinazotarajiwa kutawala ulimwengu kiuchumi kwa miaka ijayo na zote zipo katika nchi kumi za juu zilizo na watu wengi zaidi, ikionyesha umuhimu wa ukubwa wa watu wao ukiendana kabisa na ukuaji wao wa kiuchumi yaani kuna uwiano  kati ya uchumi wao na wingi wa watu wao.

Kwa mujibu wa jarida la World of Statistics mataifa matano yanatajwa kuwa na utofauti mkubwa kati ya wingi wa watu na ukuaji wa uchumi wao hasa katika ukuaji wa viwanda kulingana na idadi ya watu wao.

Mataifa ambayo yapo kwenye orodha ya nchi 10 zenye watu wengi zaidi ni  Urusi, Brazil, China na Marekani vilevile yanakuwa sana kiuchumi kulingana na idadi kubwa ya nguvu kazi au rasilimali watu.


Pia mataifa kama Indonesia,Nigeria,Bangladesh,Pakistan na Mexico kiuchumi hayajakuwa sana lakini yana watu wengi sana kitu kinachotajwa kuwa wingi wa watu haujaendana na ukuaji wa uchumi katika mataifa yao.

Zifahamu nchi hizo 10 zenye watu wengi zaidi duniani.

1. China  1,451,875,250

2. India  1,411,091,226

3. USA  335,407,012

4. Indonesia  280,162,730

5. Pakistan  230,953,560

6. Nigeria  218,286,375

7. Brazil  215,998,823

8. Bangladesh  168,449,149

9. Russia  146,074,197

10. Mexico  132,041,468.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Habiba Mohamed

A digital journalist and writer for mwananchi scoop My stories around entertainment,fashion, Artist profile, relationship, lifestyle and career.


Latest Post