Drake hatoimba tena wimbo aliofanya na Rihanna

Drake hatoimba tena wimbo aliofanya na Rihanna

‘Rapa’ kutoka nchini Marekani, #Drake akiwa katika onesho lake la ‘Its All a Blur- Big as the What’ siku ya Jumamosi nchini humo aliwaeleza mashabiki wake kuwa hatoimba tena wimbo aliofanya na #Rihanna ‘Work’ (2017) kwenye show zake.

Drake amedai hawezi kuimba wimbo huo labda mashabiki wamuimbie yeye, licha yakuwa mpaka sasa haijabainika kwa nini Drake amekataa kuimba wimbo huo aliofanya na #Rihanna.

Ikumbukwe wawili hao waliwahi kuhusishwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kabla ya Rihanna kuanzisha mahusiano na ‘rapa’ #ASAPRock.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post