Diamond sasa ni yanga

Diamond sasa ni yanga

Ooooooh!  wanaachiiii wananchiii wananchiii nimewaita mara tatu mmemfanya nini huyu kijana mpaka kuwakubali kiasi hicho, basi bwana msanii Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa yeye ni shabiki wa klabu ya Yanga kwani amemfuata Haji Manara, awali wote walikuwa mashabiki wa klabu ya Simba.

Kauli hii ameitoa jana katika siku ya kuzaliwa ya semaji la mabingwa Haji Manara, semaji hilo bwana alikukaa kimya akaamua kufunguka na kusema Yanga wakimtumia vizuri Msanii huyo ataleta faida kubwa sana, kwani mashabiki zake wengi ambao sio mashabiki wa Yanga nao watahamia Yanga.

Wooooiiiiiih! Haya haya wananchi  vipi tumkaribishe kwenye chama au tumuache kidogo, embu dondosha komenti yako hapo chini mwanangu sana.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post