Wema Sepetu Ampa Makavu Bob Junior

Wema Sepetu Ampa Makavu Bob Junior

Ukisikia kimeumana!! ndiyo hiki hapa kilichomkuta Bob Junior ambapo Madam Wema Sepetu ameamua kuvunja ukimya na kuonesha  kutopendezwa na maneno aliyoyazungumza msanii huyo.

 Nikukumbushe tu kuwa awali Bob Junior alizungumza kuwa Wema ni mwanamke wake na anataka kumtolea posa wakati akihojiwa na kituo kimoja cha redio.

Wema amekanusha madai ya taarifa hiyo baada ya kushea ujumbe mzito aliouandika kupitia ukurasa wake wa Instagram.

"Niko disappointed na Bob Junior sana cause maisha yangu always nimekuwa nikimchukulia as a friend na nimekuwa nikimkubali kama mwana, sasa sielewi ndugu yangu ukala nini au umeona ni sawa kwenda kuongea kuwa mimi ni mwanamke wako?”.

“Yaani ungejua nisivyopenda kuwa kwenye midomo ya watu aisee…….daaah……..”

"Nimekuwa sad saaaaanaaa maana hata sielewi namwambiaje Mwanaume wangu akanielewa.Kiukweli umenikosea sana haya posa hiyo ya wapi au ulikuwa umelewa, yaani kuna vitu vinakera sana kwa kweli"

 

 


 

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post