Nguli wa muziki wa Hip-hop nchini, Webiro Wassira 'Wakazi' amesema kuboresha maisha na tabia binafsi inaweza kuwa njia bora ya kuibua wasanii watakaoweza kutumbuiza live kwenye majukwaa.
Akizungumza katika mdahalo wa tamasha la HipHop Asili, uliojadili namna ya kuinua kiwango cha taaluma kwa wasanii wa HipHop, Wakazi alisema, “Tanzania tunalo tatizo la ukosefu wa taaluma ya kazi miongoni mwa wasanii. Njia moja ya kuboresha hili ni kurejea darasani na kujifunza mambo sahihi,” amesema.
Wakazi ameongezea kwa kusema kufanya mazoezi mara kwa mara na kuwa na uwezo wa kukumbuka mashairi yao ndilo chimbuko la maendeleo ya kazi zao.
“Ukiweka juhudi kwenye kujiboresha binafsi, taaluma huja kwa urahisi. Ni muhimu sana kuelewa uko wapi na uweze kuamua unataka kwenda wapi na kwa kiwango gani,” amesema
Aidha msanii huyo ambaye alitumbuzia katika tamasha hilo usiku wa Juni 27,2025 alifunguka kuhusiana na baadhi ya mashabiki kumnanga kuwa hana mwelekeo.
“Watu wananiambia, ‘Wakazi mbona huna ngoma kali (hits)?’ Mimi huwa nawauliza, je, unajua sababu gani nilianza kurap? Wewe unataka niwe kitu ambacho mimi sitaki kuwa. Mimi nafanya haya kwa ajili ya tamaduni (culture) na hicho ndicho ninachotaka kufanya.
“Hii inaturudisha nyuma sana kwenye hatua ya kwenda juu. Hatujifunzi misingi. Ndiyo maana wasanii wakubwa nchini hawawezi kufanya kile Frida anafanya au kile ninachofanya, kwa sababu wanataka vitu vya haraka,” amesema Wakazi
Leave a Reply